BACK TO LIST

باب المدّ

Mlango wa madda

 

Herufi za madda ni tatu nazo ni:         ا ، و ، ي

  • Alif =yenye sukun (yaani iliyokuwa haina kitu) herufi ya nyuma yake ikawa na fat-ha
  • Waw = yenye sukun (yaani iliyokuwa haina kitu) herufi ya nyuma yake ikawa na dhammah
  • Yee = yenye sukun (yaani iliyokuwa haina kitu) herufi ya nyuma yake ikawa na kasrah

Zimekusanywa kwenye neno hili: نُوحِيهَا

Text Box: Harakah za kuvuta huhisabiwa kwa kutumia vidole.
Na kwa ufahamu a huko kuvuta, hapa tumeikadiria harakah kimaandishi kama ifuatavyo:-
HARAKAH moja ya Alif           =         A          -moja
HARAKAH moja ya Waw         =         U          -moja
HARAKAH moja ya Yee           =         I           -moja
 
 

 

 

 

 

 

 

 


 

Madda ni kuirefusha sauti ya herufi ya madda (kama tulivyokwishazitaja hapo juu).

Herufi ya madda huzidi kuvutwa inapokutana mbele yake na hamza au sukun.

 

Madda zimegawika katika makundi mawili makuu

1-   Madda ya asili na                                الْمَدُّ الاَصْلِيّ

2-   Madda iliyozidi                    الْمَدُّ الْفَرْعِيُّ                                 

 

 

Madda ya asili

                               الْمَدُّ الاَصْلِيُّ au اَلْمَدُّ الطَّبِيعِيُّ

 

Madda hii inakuwa kwenye ile herufi yenyewe ya madda ambayo kama haijavutwa herufi hiyo ya madda basi inakuwa madda haijapatikana bado na huenda isilete maana ya hilo neno. Madda ya asili haitanguliwi baada yake na hamza wala sukun.

Mfano: قَالَ،  = qaAAla,      يَقُوْلُ = yaquUUlu,   قِيْلَ  = qiIIla

 

Makadirio ya kuivuta kwake ni harakah mbili kama tulivyoona katika mfano, ikiwa katika hali ya kupita (wasl) au kusimama (waqf), hakuzidishwi kuvutwa kwake wala hakupunguzwi. Na ndio maana ikaitwa madda ya asili.

 

2-Madda iliyozidi (ya ziyada)       الْمَدُّ الْفَرْعِيُّ                    

 

Hii ni madda inayovutwa zaidi kuliko ile madda ya asili kwa sababu ya kutokea (a) hamza, au (b) sukun baada ya herufi ya madda.

 

 

 

1 2
    Site Meter