Hukmu za
nūni iliyokuwa săkinah
نْ
na tanween ً ٍ ٌٌ
Nuni
iliyokuwa
săkinah na tanween ina hali nne nazo ni:-
IDH-HAR
IDGHAM
IQLAB
IKHFAA
IDH-HAR
Idh-har katika somo hili maana yake ni kuidhihirisha kimatamshi nuni
yenye sukun (nuni sakna) au tanween kwa kuitoa kwenye matokeo yake
khasa kama hivi “ nnn” bila ya kuitia ghunnah (Ghunnah ni sauti
itokayo puani).
Nuni
hiyo au tanween itadhihirishwa ikiwa mbele yake itatokea herufi kati
ya herufi 6 za Idh-har (zenye fat-ha kasra au dhamma) nazo ni :-
Hamza
ء
Haa
هـ
A’yn
ع
Haa
ح
Ghayn
غ
Khaa
خ
Kwa
urahisi wa kuzikumbuka herufi hizi, ziko mwanzo wa kila neno kwenye
beti hii ya ushairi:-
أََخِي
هَاكَ عِلْمًا
حَا زَهُ غَيرُ
خَاسِر
Sasa Tuangalie
mifano ili tupate kujuwa namna gani tunaweza kuitambua hii hukmu ya
Idh-har.
Kwanza tufahamu
kwamba nuni yenye sukun (sakna) hutokezea kwenye neno moja au maneno
mawili tofauti kama tutakavyoona kwenye mithali:-
مَنْأ ٰ مَنَ
Kwa hiyo hapa
tutadhihirisha nuni săkinah kwa sababu mbele yake ipo alif nayo ni
herufi ya Idh-har. Tunasoma bila ya kutia ghunnah